Wednesday, August 20, 2014

Bodi ya DAWASA yatembele Mirani ya Maji Ruvu chini na Ruvu juu leo

Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) leo Agosti 20,2014 imefanya ziara ya kutembelea Miradi yao ya Maji ya Ruvu Juu na Ruvu Chini ili kujionea maendeleo ya ukarabati wa Miradi hiyo miwili ambayo ilikuwa katika ukarabati.Katika ziara hiyo Bodi hiyo ya DAWASA imeridhishwa na upanuzi wa Mtambo wa Maji wa Ruvu chini ambao kwa sasa umekamilika kabisa huku ukiwa na uhakika wa kutoa maji ujazo wa Lita Milioni 270 kwa siku.

 Pichani ni Bango la Mkandarasi anaejenga Visima na kukarabati Mabomba ya Maji ikiwa ni Kituo kitakachosambaza maji katika maeneo mbali mbali ya Jiji la Dar es Salaam kutoka kwenye Mitambo ya Ruvu Juu,eneo hili lipo Kibamba,Jijini Dar es salaam.
 Meneja Miradi wa Kampuni ya Megha Engineering & Infrastructures Ltd ya nchini India,Murali Mohan (mwenye kizibao cha kijani) ambao ni wakandarasi wa Ujenzi wa Visima na Ukarabati wa Mabomba ya Maji ya DAWASA katika eneo la Kibamba,akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Bodi ya Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) ambayo iko chini ya Mwenyekiti wake,Dkt. Eve-Hawa Sinare (wa tatu kushoto) wakati walipopita kwenye Mradi huo utakaosambaza maji kutoka kwenye Mitambo ya Ruvu Juu.Picha zote na Othman Michuzi.
 Meneja Miradi wa Kampuni ya WABAG India,Pintu Dutta (wa pili kushoto) akieleza jambo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA),Dkt. Eve-Hawa Sinare (wa tatu kushoto) alieambatana na wajumbe wa Bodi hiyo wakati wa ziara yao ya kutembelea Mradi wa Maji wa Ruvu Juu unaonendelea na ukarabati hivi sasa.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA),Dkt. Eve-Hawa Sinare (alienyoosha mkono) akielekeza kitu wakati akiangalia ujenzi wa nyumba za Wafanyakazi wa DAWASA watakaokuwa wanaendesha miradi hiyo ya Maji Ruvu Juu.
 Meneja Miradi wa DAWASA,Ing. Romanus Mwang'ngo (kulia) akiwaonyesha kitu Wajumbe wa Bodi ya DAWASA waliofanya ziara ya kutembelea Mirani ya Ruvu Juu na Ruvu Chini leo Agosti 20,2014.
Ziara ikiendelea.

Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA),Ing. Archerd Mutalemwa akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya namna Shirika lake lilivyojipanga kuwaondolea kabisha hadha ya maji Wakazi wa Jijini la Dar es Salaam wakati akielezea kukamilika kwa Mtambo wa Maji wa Ruvu chini wenye Uwezo wa kutoa maji Lita Milioni 270 kwa siku ukitofautisha na uwezo wa Mtambo wa zamani uliokuwa ukitoa lita chache. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA),Dkt. Eve-Hawa Sinare akizungumza na waandishi wa habari juu ya ziara yake hiyo aliyoambatana na Wajumbe wake wote.
 Mhandishi Mshauri wa Kampuni ya UWP,Chacha Wambura (mwenye kizibao cha rangi ya chungwa) akitoa maelezo ya Maendeleo ya Mradi wa Ruvu chini kwa Ujumbe wa Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) uliotembelea Mradi huo leo Agosti 2014.
 Sehemu ya Mabomba ya kusafirishia Maji katika Mtambo wa Ruvu chini.
  Mhandishi Mshauri wa Kampuni ya UWP,Chacha Wambura akifafanua jambo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA),Dkt. Eve-Hawa Sinare wakati wakitembelea sehemu ya Mtambo wa Maji wa Ruvu chini uliomalizika matengenezo yake.
Sehemu ya visima vya Maji Ruvu chini.
 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA),Alhaji Said El-Maamry (kushoto) akiuliza jambo kwa Meneja Miradi wa DAWASA,Ing. Romanus Mwang'ngo (kulia) juu ya Mtambo wa Ruvu chini,wakati wa ziara yao iliyofanyika leo Agosti 20,2014.Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo,Dkt. Eve-Hawa Sinare
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA),Dkt. Eve-Hawa Sinare (wa pili kushoto) akijadiliana jambo na Makamu wake,Alhaji Said El-Maamry (kulia) mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea miradi ya Ruvu Juu na Ruvu chini leo Agosti 20,2014.Wengine pichani ni Wajumbe wa Bodi hiyo,Bw. Daniel Machemba (kushoto) na Ing. Mary Mbowe (wa pili kulia)
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumaliza ziara yao katika Miradi ya Ruvu Juu na Ruvu chini leo.


No comments: